Shukurani

3 views

Lyrics

Nina kushukuru Mungu sababu ya mengi, hata uhai huu sikustahili
 Nina kushukuru Mungu tena sababu ya vingi, hata nikiwa nasali unajua namaanisha
 Sio kama eti nilitenda wema wakuja linganisha na matendo yako makuu mimi Mungu ningekulipa nini
 Ulikonitoa ni siri ya moyo wangu matopeni topeni ukaniketisha na wakuu juu
 Umenipa heshima ukanifuta machozi asante ooh baba
 Hata shukurani zangu ni kwako
 Shukrani zangu ni kwako
 Na shukurani zangu ni kwako
 Shukurani zangu ni kwako, asante baba ooh
 Aibu umefuta fedheha umefuta
 Umenipa amani iliyo ya kweli nakumbuka nalia mimi ni yule ambae
 Nilitukanwa na kwa dharau wakasema kwisha habari yake kuna kipindi nilikufa nikawa mifupa inayotembea
 Ikiwa kwa siku za usoni walisema tunazika kesho
 Ila kwa huruma uliniponya na kaburi kwa hurumaa na sitosahau wema wako wee baba
 Hata shukurani zangu ni kwako
 Shukrani zangu ni kwako
 Na shukurani zangu ni kwako
 Shukurani zangu ni kwako, asante baba ooh
 Kama kusoma tumesoma wengi umeruhusu niwe na kazi nzuri
 Ajali tulipata wengi umeruhusu nibaki nauzima (asante Baba)
 Ndoa zilifungwa nyingi umeruhusu tubaki na amani
 Furaha wanakosa wengi umeruhusu tabasamu kwangu
 Na shukurani zangu
 Yelele, yelele mama, yelele mama, yelele mama, yelele
 Yelele, yelele mama, yelele mama, yelele mama yelele
 Yelele, yelele mama, yelele mama, yelele mama yelele
 Yelele, yelele mama, yelele mama, yelele mama yelele
 Yelele, yelele mama, yelele mama, yelele mama yelele
 Yelele, yelele mama, yelele mama, yelele mama yelele
 Yelele, yelele mama, yelele mama, yelele mama yelele
 Yelele, yelele mama, yelele mama, yelele mama yelele
 

Audio Features

Song Details

Duration
04:39
Key
4
Tempo
93 BPM

Share

More Songs by Goodluck Gozbert

Similar Songs