Enda Nasi

3 views

Lyrics

Hufika wakati katika maisha ya binadamu ambapo tunafanya mambo bila ya Mungu kuwa nasi
 Ni vema kufahamu kwamba asipoenda nasi, haitawezekana sisi kufaulu
 Kama Musa nawa Israeli, tuombe Bwana tafadhali, enda nasi
 Hili liwe ni ombi lako siku ya leo
 ♪
 Tunaomba uwepo wako uende nasi
 Ewe bwana wa majeshi tusikie
 Kama huendi nasi, hatutaki kutoka hapa
 Hatuwezi peke yetu, enda nasi
 Tu watu wa shingo ngumu tusamehe
 Hatufai mbele zako turehemu (tusafishe)
 Tusafishe e baba, tuonyeshe uso wako
 Twahitaji neema yako, enda nasi (mm-hm)
 Tutavua, mapambo yetu
 Vitu vyote vya dhamani kwetu (mioyo yetu)
 Mioyo yetu twaleta mbele zako
 Tutakase na utembee nasi
 Tunaomba utuonyeshe njia zako (kwa maana)
 Kwa maana umetuita kwa jina lako
 Twalilia e bwana, utukufu na uso wako
 Bila wewe tutashindwa, enda nasi
 Oh, Bwana
 Tutavua, mapambo yetu
 Vitu vyote vya dhamani kwetu
 Mioyo yetu twaleta mbele zako
 Tutakase na utembee nasi
 Ndugu na dada yangu, tafadhali
 Usijaribu kuyamudu maisha bila yake Bwana, utashindwa
 Yafaa tufike mahali ambapo Musa alimlilia bwana na kutafuta uso wake
 Na kusema, "Bwana tafadhali, enda nami, enda nasi, twakuhitaji" whoa
 Tutavua (tutavua), mapambo yetu (mapambo yetu)
 Vitu vyote vya dhamani kwetu
 Mioyo yetu twaleta mbele zako (twaleta Baba)
 Tutakase na utembee nasi (tutavua)
 Tutavua, mapambo yetu
 Vitu vyote vya dhamani kwetu
 Mioyo yetu twaleta mbele zako
 Tutakase na utembee nasi
 Mioyo yetu twaleta mbele zako
 Tutakase na utembee nasi (mioyo yetu)
 Mioyo yetu twaleta mbele zako (tuna leta mbele zako)
 Tutakase na utembee nasi
 Oh, Bwana, tembea nasi
 Bila wewe tutashindwa
 Hili ni ombi letu, Baba
 

Audio Features

Song Details

Duration
05:21
Key
8
Tempo
136 BPM

Share

More Songs by Reuben Kigame

Similar Songs