Sayari

3 views

Lyrics

Stanza1
 Sayari... sayari... eeh dunia
 mbona wanipa hofu nyingi ewe dunia
 yatokeao kwako ewe dunia
 Kila kukicha mambo hugeuka kuwa maongo
 inawezekana umezeeka dunia
 au wakaao ndani yako ndio wamezeeka
 Kila ufikapo ni vilio nifanyeaje
 maafayawakabili wengi dunia wazeeka
 Sayari dunia uliumbwa wapendeza
 lakini sasa watupeleka wapi
 tunahangaika hatujui tuendako
 ni mungu pekee ajuaye
 Stanza 2
 njaa majonjwa yasiyotibika
 mambo yatisha eeh dunia waenda wapi
 kila mahali ni jangwa twende wapi
 rotuba nayo imeshatoweka sasa twende wapi
 hali ya maisha ni ngumu sana kwa wote
 kwa tajiri na maskini wote nisawa
 uchumi wa dunia yote wayumbaa
 ona mataifa makubwa yote nayo yajejereka
 sayari dunia uliumbwa wapendeza
 lakini sasa watupeleka wapi
 tunahangaika hatujui tuendakako
 ni mungu pekee ajuaye
 Stanza 3
 sayari dunia umechoka
 na wakao ndani yao wote wamekuchoka
 hakuna mzazi awezae kuvumilia
 Kuona mwanawe anakatwa kichwa kwa ajili ya kafara
 damu za watu zimekua ni tamu
 nionavyo si kawaida ewe dunia
 tuyaonayo yanatisha dunia
 oooh nahofu moyoni mwangu
 sayari dunia uliumbwa wapendeza
 lakini sasa watupeleka wapi
 tunahangaika hatujui tuendako
 ni mungu pekee ajuaye
 tunahangaika hatujui tuendako
 ni mungu pekee ajuaye
 (repeat)
 Lyrics by Ndeche Herman

Audio Features

Song Details

Duration
06:07
Key
3
Tempo
82 BPM

Share

More Songs by Ambassadors Of Christ Choir

Similar Songs